Call for participants | Generation Food Accelerator | CLOSED

Call for participants | Generation Food Accelerator | CLOSED

04/06/2021
in News
Applications open until 19.07.2021

Applications open until 19.07.2021

Apply here for the Generation Food Accelerator. More information below.

Apply here

[ENGLISH VERSION BELOW]

Mwito wa usaili kushiriki mradi wa Vijana na Wanawake wa Generation Food Accelerator

Je, wewe ni mjasiriamali kijana na mwenye shauku ya kuunda suluhisho jipya na bunifu ili kuhakikisha uendelevu na ujumuishaji katika mfumo wa chakula katika Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania? Una biashara au unatarajia kuanzisha biashara katika sekta ya matunda na mboga? Wewe ni mkulima mwenye msukumo, mtoa huduma mwenye maono, mtendaji kazi mbunifu, au labda wewe ni mpishi unayependa lishe?

Jisajili sasa kwa mradi wa Generation Food Accelerator! Tunatafuta wafanyabiashara mbalimbali wanaojihusisha haswa katika mnyororo wa thamani wa kilimo cha matunda na mboga, kwani uwezekano wa kuchangia mfumo endelevu wa chakula unaojumuisha watu wote, hauna kikomo.

Programu inahusika na nini?

Generation Food Accelerator ni mradi unaosimamiwa na kuendeshwa na shirika la Rikolto Africa Mashariki kwa kushirikiana na Sahara Ventures, kupitia ufadhili wa Umoja wa Nchi za Ulaya, chini ya programu kubwa ya AGRI-CONNECT.

Generation Food Accelerator ni mradi uliojikita katika kuibua na kuboresha biashara bunifu zinazolenga mnyororo wa thamani wa mifumo ya chakula kutoka mikoa ya Nyanda za Juu Kusini hususani: Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe and Katavi. Mradi huu unajikita katika kutambua vijana wajasiriamali na wengineo wenye mawazo bunifu ya kibiashara yanayoweza kuendeleza na kukuza usawa wa mnyororo wa thamani wa mifumo ya chakula katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini,Tanzania.

Mradi unatarajia kusaili biashara mia moja (100), biashara ishirini (20) kila moja kutoka mikoa mitano (5) ya Nyanda za Juu Kusini (Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe, and Katavi) kuwa wanufaikaji wa mradi huu. Katika mradi huu, washiriki watapata mafunzo ya kina kuhusu: urasimishaji wa bashara zao, ubunifu wa mtindo wa biashara, chapa na alama za biashara pamoja na utafutahi masoko, masuala ya kodi na kisheria kuhusiana na biashara zao, na nafasi ya kukutana na wajasiriamali waliofanikiwa katika sekta yao kwenye mazingira yao.

Mradi unatarajia kusaili vijana wajasiriamali wenye biashara zinalolenga kutatua changamoto zifuatazo;

  • Uzalishaji endelevu na salama wa kilimo cha mbogamboga na kilimo cha mijini(mf. kanuni bora za kilimo, matumizi sahihi ya dawa za kuua wadudu, vifaa vya umwagiliaji kwa kutumia jua, teknolojia bunifu, kilimo cha mboga zilizosahaulika na matunda yenye kiwango cha juu cha virutubisho)
  • Utunzaji endelevu na bunifu, ufungaji, usambazaji, usindikaji na kupunguza uaribifu wa mazao ya mbogamboga kwenye mnyororo wote wa thamani baada ya mavuno. (mf.majokofu ya kwenye masoko, Usindikaji wa juisi/supu kutoka uzalishaji wa hali ya chini, usaifir wa umeme, Mboji)
  • Utoaji endelevu na jumuishi wa vyakula, kuhakikisha vyakula vyenye afya na lishe vinapatikana kwa watu wote. (mf. Migahawa yenye chakul safi na bora, Utoaji wa lishe bora mashuleni)

Mtiririko wa Mradi wa Generation Food Accelerator

a. Kufunguliwa kwa usaili

  • Mwisho wa kupokea maombi ya usaili: 19.07.2021

b. Mafunzo Kambini

  • Biashara 100 (Biashara 20 kila mkoa) zitachaguliwa
  • Siku 5 kila mkoa kutoa mafunzo ya kinaya biashara na kukutana na wataalamu mbalimbali.

c. Acceleration

  • Biashara 25 (Biashara 5 kila mkoa) zitachaguliwa
  • Mafunzo kwa miezi 3
  • Mafunzo ya binafsi na ushauri wa kibiashara

d. Siku ya Maonyesho

  • Biashara 15 (Biashara 3 kila mkoa) zitapatiwa mitaji
  • Nafasi ya kukutana na watalaamu na wafanyabiashara mbalimbali.

Nani anaweza kushiriki?

Unaweza kushiriki kwenye program huu endapo;

  • Wewe ni binti au kijana wa kiume mwenye umri kati ya 18-35,
  • Unatoka katika vijiji au maeneo ya mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ifuatayo: Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe and Katavi.
  • Unashauku ya kuanzisha biashara binafsi hasa kwenye sekta ya mboga na matunda kusini mwa Tanzania.

Je, umevutiwa na mradi huu? jiandikishe sasa! Kushiriki ni bure kabisa.

Kwa namna gani ujisajili?

Ingia kwenye kiunganishi hiki cha mtandao kisha Jaza fomu hii, mpaka kufikia tarehe 19 Julai 2021 saa 5:59 usiku. Endapo unakutana na changamoto katika kujiandikisha tafadhali wasiliana na Emmanuel Senzighe kupitia Barua pepe: senzighe [at] saharaventures.com au kwa simu nambari: 0744 828241.

Endelea kufuatilia mradi huu kupitia kurasa zetu za Instagram na Facebook kwa jina la: @generationfood.tanzania #GenerationFoodAccelerator

Tafadhali zingatia kuwa tutachukua hatua stahiki dhidi ya COVID-19 katika kulinda usalama wako wakati wa mradi wetu.


Call for Participants | Generation Food Accelerator

Are you a young and passionate food entrepreneur, who wants to create new and innovative solutions to ensure sustainability and inclusiveness in the food system in Tanzania’s Southern Highlands? Do you have a business or are you setting up a business in the fruit and vegetable sector? You are a driven farmer, a visionary service provider, an innovative processor, or maybe a chef passionate about nutrition?

Sign up for the Generation Food Accelerator! We are looking for a wide variety of entrepreneurs involved specifically in the horticulture value chain, as the possibilities to contribute to a sustainable, inclusive food system are limitless.

What is the Generation Food Accelerator?

Generation Food Accelerator is a project organised by Rikolto in East Africa together with Sahara Ventures and funded by the European Union under the AGRI-CONNECT programme.

The Generation Food Accelerator aims at identifying and supporting innovative business solutions in the horticulture value chain focused on a sustainable and inclusive food system in the Southern Highlands, specifically in the following regions: Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe, and Katavi.

The project is looking to recruit 100 starting businesses, 20 businesses each from five regions in the Southern Highlands. After the application, these businesses will be supported with intensive business coaching on compliances, business model innovation, branding & marketing, finances, tax issues, and legal issues. This opportunity will also connect young entrepreneurs with organizations that support businesses financially and offer a chance to network and connect with successful business people in the sector from their local environment.

The project is looking to recruit young entrepreneurs whose business is active in one of the following thematic areas:

  • Healthy, sustainable, and nutritious horticulture and urban farming (e.g. Good Agricultural Practices, solar-powered drip, aquaponics, innovative technologies, cultivation of ‘forgotten’ indigenous vegetables & fruit with high nutritional value)
  • Sustainable and innovative storage, packaging, distribution, food processing, and food waste management to manage horticulture produce throughout the value chain and minimize post-harvest losses (e.g. cold hubs in markets, processing of juices /soup from lower-quality produce, electric transport, composting)
  • Sustainable and inclusive food provision to make healthy and nutritious food accessible to all (e.g. healthy restaurants, nutritional school feeding)

Project Pipeline

a. Call For Application (1 month)

  • Deadline: 19.07.2021

b. Bootcamp

  • 100 businesses (20 per region will be selected)
  • 5 days in each region intensive business coaching and networking

c. Acceleration

  • 25 Businesses (5 per region) join for three months
  • Personalised business coaching and mentoring

d. Demo Day

  • 15 businesses (3 per region) receiving seed funding
  • Networking opportunity with experts and experienced business people.

Who can apply?

You can apply to the Generation Food Accelerator project if:

  • you are a young woman or man between 18 and 35,
  • you come from a rural or urban area in and around Southern Highland regions (Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe, and Katavi).
  • you have a strong interest in improving your own business in the horticulture sector in the Southern Highlands.

Are you excited? Apply now! Participation is free of charge.

How to register?

Fill in our online registration form via this link by 19th July 2021, 11:59 pm.

If you experience trouble registering online then please contact Emmanuel Senzighe via Email: senzighe [at] saharaventures.com or phone: 0744 828241.

Please note we will take the necessary covid-19 measures to ensure your safety during the project.